Thursday, 23 November 2023

VODACOM TANZANIA WATOA BIMA KWA WATOTO 100 MNAZI MMOJA


NA YASSIR MKUBWA - ZANZIBAR TODAY

JUMLA ya mama 100 na watoto 100 wamepatiwa bima kubwa ya bure ya mwaka mzima na kampuni ya Teknologia na mawasiliano Vodadom Tanzania. 

Kina mama hao ni wale waliojifungua watoto wao kunazia Novemba 9 mwaka huu katika hospitali ya Rufaa Mnaznimmoja kupatiwa zawadi hiyo ya upendo. 

Akizungumza katika hafla ya kukabidhi bima hizo Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano Vodacom Tanzania, Anet Kanora, alisema hatua hiyo ni muendelezo wa kampuni hiyo kutoa zawadi kwa wateja wake ikiwa ni njia ya kuwashukuru lakini kwa mwaka huu wameona ipo haja ya kuifikia jamii pana ya watanzania.

Alisema afya ya mama na mtoto ni muhimu kwa kampuni hiyo hivyo wameona ipo haja ya kumpatia bima kubwa mama pamoja na mtoto wake itakayomuwezesha mama na mtoto wake kupata matibabu.

Aidha alisema kwa Tanzania nzima bima hiyo itanufaisha watoto 1000 na mama 1000 lakini kwa Zanzibar kinamama 100 na watoto 100 watanufaika na bima hiyo ya afya.
Alisema bima hizo zitatumika katika hospitali mbalimbali za Zanzibar ikiwemo Ampola Global, Tawakal, Alrahma na hospitali ya Rufaa Mnazimmoja kwa Zanzibar na hospitali ya Muimbili na nyengine za Tanzania bara.   

Mkuu Anet alibainisha kuwa bima hiyo itakuwa haina upendeleo kwani ni lazima watoto wote watakaozaliwa katika kipindi hichi basi wote watanufaika na bima hiyo kuona wanatibiwa magonjwa mbalimbali ikiwemo ya kulazwa ama kutibiwa na kuondoka.
Alibainisha kuwa anaamini bima hiyo itakwenda kuwasaidia wazazi na watoto wao kwani mwaka wa kwanza wa mtoto ni muhimu sana katika upimaji na upatikanaji wa afya bora katika makuzi ya mtoto.

Akizungumzia kuhusu kampeni ya ‘Sambaza Shangwe, Gusa Maisha’ Meneja Mauzo Vodacom Zanzibar, Fadhili Linga, alisema kampeni hiyo ina sehemu mbili, kwanza kuwazawadia wateja kwa zawadi mbalimbali na pili kujikita katika shughuli za kijamii.
Linga alisema sekta ya afya ni eneo muhimu na kampuni hiyo imeona iendeleze jitihada za kuunga mkono serikali kupitia miradi mbalimbali.

Aliahidi kuwa watanendeleza ushirikiano huo ili kuhakikisha upatikanaji wa huduma bora za matibabu ya afya kwa Watanzania wote zinapatikana bila ya usumbufu.
Alisema mbali na kutoa bima pia Vodacom imekuwa ikiwazawadia zawadi kama vile bodaboda, TV, simu za mkononi, router za 4G na 5G na pesa taslimu kuanzia shilingi 500,000 mpaka milioni 10,000,000.

Khadija Salum Said ni Mkuu wa Wodi ya Wazazi hospitali ya Rufaa Mmnazimmoja, aliipongeza kampuni hiyo kwa ubunifu wa kampeni hiyo ambayo inawajali kinamama wanaoleta viumbe wapya duniani.

Alisema kupatiwa bima hizo itasaidia kwa kiasi kikubwa kupatikana kwa huduma ya uhakika ya afya katika hatua ya awali ya watoto wachanga na akina mama waliotoka kujifungua na kupunguza vifo vya mama na watoto wachanga. 

Kwa kupatia bima ya afya ya bure, tena ile kubwa kwa mwaka mzima, akina mama hawa na watoto wao hawatokuwa na shaka pindi watakapokumbwa na changamoto za kiafya, ujio wenu huu umetusaidia sana kupunguza matatizo ambayo yatatokea baada ya mama kujifungua na hata kupunguza vifo vya watoto wachanga,”alisema.

Hivyo, aliiomba kampuni hiyo kuendelea kushirikiana pamoja katika mapambano ya kupunguza vifo vya mama na mtoto kwa kusaidia bima hiyo kwa wazazi wa Tanzania nzima kwani utoaji wa bima hiyo ni njia moja ya kupunguza vifo hivyo. 

Wakizungumza kwa niaba ya wazazi wenzao waliopatiwa bima hizo Maryam Yohana Daniel na Badria Mohammed Khamis aliejifungua watoto mapacha walipongeza Vodacom kwa kuwapatia bima hizo ambazo zitawasaidia kupata matibabu wao na watoto wao na huduma nyengine za kiafya.

Hivyo waliiomba jamii kujiunga na kampuni ya Vodacom ili iweze kusaidia kundi kubwa zaidi katika jamii ya watanzania. 

VodaBima itawawezesha akina mama na watoto wao kupata huduma za afya ni sehemu ya kampeni inayoendelea ya kampuni hiyo nchini kote ijulikanayo kama ‘Sambaza Shangwe, Gusa Maisha’.

MWISHO.




Tuesday, 21 November 2023

MSAADA WA KISHERIA WAWAOKOA WATOTO WANAOKINZANA NA SHERIA ZANZIBAR:

Na AMINA MCHEZO:

   Msaada wa watoto kisheria, kisera na kimipango ni uwanja mpana huku ikionekana sheria iliopo Sasa ya mtoto sheria namba 6 ya mwaka 2011 inamapungufu hivyo wizara ya Màendeleo ya jamií, jinsia, wazee na watoto Zanzibar inafanya juhudi kuhakikisha sheria hiyo inapitiwa upya.

   Sheria hiyo Kwa Sasa inaonekana bado haitoi ulinzi Bora Kwa mtoto hivyo Kwa Sasa wadau na taasisi za usimamizi wa mtoto wamekuwa wakiisindikiza tume ya marekebisho ya sheria ili kuwe na sheria mpya.
 
    "Kwa Sasa tumeshatoka kwenye hatua nyingi za ukusanyaji wa maoni ya wadau na Sasa nadhani tupo katika hatua ya kuishirikisha tume ya marekebisho ya sheria ili tuone kwamba tunapata baraka za mwisho na kunipeleka mbele ili tuwe na sheria mpya ili mambo yawe mazur Kwa watoto" Amesema mkuu wa wa Division  ya hifadhi ya mtoto kupitia idara ya ustawi wa jamii na wazee.

   Mtoto anaekinzana na sheria ni mtoto yeyote alie chini ya umri wa miaka 18 ambae amefanya makosa ya kijinai ikiwemo kubaka, kulawiti, wizi na makosa mengine.
 
  Utafiti umebaini kuwa watoto wengi wanaokinzana na Sheria ni wale watoto wa mzazi mmoja, ndoa kuvunjika, Kukosa matunzo Kwa wazazi wake, hivyo watoto hao hupelekea kuathirika kiakili Kwa kujiingiza katika  makundi maovu na kufanya makosa ya kijinai.

   Kiuhalisia kutokana na sababu hizo inaonekana wazi watoto wanaokinzana na sheria wengi wao ni wale waliopitia udhalilishaji Kwa namna Moja au nyengine kutokana na Kukosa malezi sahihi na Kukosa haki zake za msingi kama mtoto.

    Msaada wa kisheria Kwa watoto wanaokinzana na sheria umeibua hisia tofauti Kwa wanajamii hasa pale wanapoona makosa ya namna hiyo yakijirudia Kila mara
     
     Wengine wanasema kupatiwa msaada wa kisheria ni sawa tu kwani wale ni watoto mengi wanayafanya Kwa kutokujua.
   
     Huku mitazamo ya wengine yakionekana kubeba hisia Kali na kukataa kabisa watoto wale kupewa msaada wakidai kuwa ni njia Moja ya watoto hao kuendelea kutenda makosa Kila siku.

     "Sioni sababu ya watoto wanaotenda makosa kupewa msaada wa kisheria  kwani nao wanajielewa na wakisaidiwa  kisheria yaani watoto watakuwa wanajiamini Sana" Wamesema baadhi yao.

      Mtumwa Ameir Ali msaidizi wa sheria kutoka wilaya ya mjini amesema bado baadhi ya  wanajamii hawajaelewa kuhusu kutolewa Kwa msaada wa kisheria Kwa watoto wanaokinzana na sheria.

      Amesema ushawishi wao ni mkubwa Kwa kutafuta wakili wa usimamizi wa kesi za watoto pamoja na wao kumpa elimu na ushauri ili asirudie tena kosa Lile.

     Amefahamisha kuwa kumuacha mtoto aliekinzana na sheria ni kumkosesha haki zake za msingi ikiwemo kusoma pindi tu atakapokaa chuo Cha mafunzo Kwa Kukosa usaidizi wa kisheria.
    
     "Baadhi ya wajamii hawana uwelewa Kwa sababu wanaona yule mtoto ameshatenda Lile kosa kwanini sisi tunakaa tunamtetea lakini jamii hawajui kuwa Lile kosa linaweza kuwa lisiwe lake au amefanya kosa Kwa ule utoto tu." amesema.

     Bi mtumwa amesema ijapokuwa wao sheria inawabana kuingia mahakamani lakini hawawezi kumuacha mtoto aliekinzana na sheria hivyo wanaanza ngazi za awali ikiwemo polisi ili apate haki yake Kwa wepesi na haraka. 

    Jumla ya kesi 129 zimeripotiwa katika mahakama tofauti visiwani Zanzibar kuanzia January Hadi November 2023 zinazowahusu watoto waliokinzana na sheria ,  Kwa mujibu wa kitengo Cha TAKWIMU Dawati la Jinsia Makao Makuu ya polisi Zanzibar.

    Ambapo kesi 70 ni Kwa mkoa wa mjini magharib, 8 mkoa wa kusini unguja, 21 Kwa mkoa wa kaskazini unguja, 16 Kwa mkoa wa kusini Pemba na kesi 14 Kwa mkoa wa kaskazini Pemba.

   Akizungumza na mwandishi wa makala hii mratibu  wa Dawati la  jinsia makao makuu ya polis Zanzibar Sajent Rahma Ali Salum amesema watoto wanaokinzana na sheria wanawaangalia kama watoto wengine hasa katika kuwasaidia Kwa kuwapatia elimu ya kujitambua.

   Amesema  katika usaidizi wao wa kisheria Kwa watoto wa namna hii wanashirikiana na wasaidizi wa sheria, waratibu wa shehia pamoja na ustawi wa jamii  Kwa kusikiliza kesi zao Kwa  pamoja.

     Sagent Rahma amefahamisha kuwa  ni wajibu wa watoto wanaokinzana na sheria kupatiwa msaada kutokana na mazingira yanayojitokeza wakati wanapofanya makosa.

    "Tikifuatilia kesi zao nyingi ni ushawishi wa watoto wezao, wengine kuwa na njaa kutokana na Kukosa chakula nyumbani ilimradi makosa yao mengi ni ya ushawishitu" Amesema Sagent Rahma.

   Amesema Dawati la jinsia wanapopokea kesi za watoto waliotenda makosa wanawaita wazazi wao kuwafahamisha namna ya kukaa na mtoto wake kwani wazazi wengi huwachukia watoto wao kutokana na makosa yao.

   " Msaada wa kisheria Sana wanapewa na wasaidizi wa sheria wanakuwa pamoja na wazazi wao sisi tunawafahamisha namna Yale makosa yalivyo na mtoto akaenae vipi Kwa sababu wazazi wengine  wanakuwa wakali na kimchukia "Amesema.

       Amefahamisha kuwa katika kuwasaidia watoto wamekuwa wakipelekwa katika mahakama ya watoto ili wapate uhuru wa kujieleza mbele ya mahakama.

    Jumuiya ya wanasheria wanawake Zanzibar ZAFELA ni jumuiya isiyo ya kiserikali ambayo inatoa msaada wa kisheria Kwa wanawake na watoto imesema Kuanzia January Hadi November 2023 jumla ya kesi 11 za watoto wanaokinzana na sheria  zimefika ofisini kwao na wameanza  kuzishughulikia Kwa kuwapatia msaada wa kisheria na kesi 3 tayar zimeshapatiwa ufumbuzi Kwa kutozwa faini.

   Mwanaisha Mustapha ni mwanasheria kutoka jumuiya ya wanasheria wanawake Zanzibar ZAFELA amesema Kwa watoto wanaokinzana na sheria wamekuwa wakiwasimamia Kwa hali ya juu kwani wengi wao makosa yao ni ya kusingiziwa au ya kulipiziwa visasi Kwa baadhi ya wanajamii waliomzunguka.

    Amesema wao kama wanasheria wanasimama kwenye sheria ya mtoto inavyozungumza katika kumlinda kama mtoto mwengine mpaka pale mahakama itakapomtia hatiani Kwa kosa Lile.

    Amefahamisha kuwa hali ya Sasa asilimia kubwa watoto Kwa watoto wanafanyiana udhalilishaji jambo ambalo wanataasisi zinazotoa msaada wa kisheria wamekuwa macho ili  jamii ibaki kuwa salama.

   "Ni janga kubwa hali ya udhalilishaji na hali ya Sasa hivi iliokuwepo asilimia kubwa watoto Kwa watoto ndio wengi ambao wanafanya haya matukio Kwa iyo tukiwaangali kisheria wote ni watoto na wote wanataka kulindwa na sheria" Amesema mwanasheria.

    Shirika la msaada wa kisheria nà haki za binaadam  Zanzibar ZALHO kupitia wakili wake bi Jamila massoud  amesema jumla ya kesi 19 wanazishuhulikia katika shirika lao huku kesi 7 zikiwa zimeshafikishwa mahakamani Vuga zinazowahusu watoto wanaokinzana na sheria.

    Amesema  shirika limekuwa na utaratibu wa kuandaa mikutano na wanajamii ili kuzungumza nao na kuwafahamisha kwanini watoto waliokinzana na sheria wanatakiwa kupatiwa msaada wa kisheria.

   Amebainisha kuwa pale wanaposhughulikia kesi za watoto wanaokinzana na sheria wanashauri Sana kubadilishiwa makaazi pale anapokuwa tayar ameshakuwa mtoto mwema kwenye jamii ili asirudia tena makosa yale.

    "Tunawapa muelekeo au tunawapa utaalamu kwanini tunawasaidia hawa watoto Kwa sababu hawa ni Victim wa udhalilishaji ukiangalia mtoto anaekinzana na sheria utagundua kuwa nae kadhalilishwa Kwa namna Moja au nyengine" Amesema.

      Mohd Khamis Faki mkaazi wa kazole anaemlea mtoto wa dada yake  ajulikanae Kwa jina Khamis Mwadini Kheir mwenye umri wa  miaka 16 alishtumiwa Kwa kosa la kukashifu mtoto wa kike mwenye umri wa miaka 16 mnamo mwezi wa march 2023 huko maeneo ya Daraja bovu wilaya ya maghari A unguja.

     Katika shtaka Hilo lililopekea kufikishwa kituo Cha polisi Mwera na kesi kupelekwa mahakamani Vuga mjini unguja, ndugu Mohd Khamis amesema baada ya kufikishwa mahakamani shtaka la mjomba wake awali walishindwa Kwa Kukosa wakili kutokana na hali yao ya kimaisha.

      "Tulipandishwa mahakamani Vuga tulishindwa kupata wakili kutokana na hali zetu ndipo tukaunganishwa na Mtu kwenye hili shirika hili pale mikunguni linalosaidia watu wasio na uwezo na Kwa uwezo wa Mwnyezi Mungu Lile shirika lilitusaidia mpaka kesi ilipomalizika na alhamdullillah hatukutozwa  ushuru wowote ule" Ameongeza

      Amesema msaada walioupata kutoka shirika la ZALHO ni mkubwa kwani walishindwa na fedha za kuwapa wakili ili kuwasaidia kesi ya mjomba wake na Kwa Sasa mjomba wake huyo yupo huru na amejifunza kutokana na kosa Lile pamoja na kimkataza kufika katika mtaa aliopatia mtihani huo.

     "Kwa Sasa tumempiga Marufuku kufika mitaa ya Daraja bovu ambako ndipo alipo huyo binty kwenye hiyo nyumba aliofika mjomba wangu na Kwa Sasa hata hasogei kwani ulikuwa ni mtihani tu ule kwake" Amesema.

    Wizara ya Màendeleo ya jamií, jinsia wazee na watoto Zanzibar imesema hali ya upatikanaji huduma kisheria Kwa watoto ni ndogo na ndio maana wameona Kuna haja ya kutia mkono sheria iliopo Sasa ili kuboreshwa Kwa huduma.

   Mkuu wa Division ya hifadhi ya mtoto idara ya ustawi wa jamii na wazee ndugu sheikh Ali Sheikh amesema watoto wanaokizana na sheria sheria bado inamtanzama kama mtoto mbali ya kuwa wanatenda makosa lakini sheria inataka kuwalinda pia na kupewa haki zao.

   Amesema kama idara inatoa msaada wa kisheria Kwa kuwasimamia mahakamani hadi pale hukumu zinapotokea ambazo kikawaida ni kutozwa faini tu na sio kufungwa baadae idara inawapeleka vituo vya kurekebisha tabia kwenda kupata ujunzi na kujiweka sawa.

   "Tunamsaidia kama mtoto kama sheria inavyotaka atizamwe Kwa hiyo Kuna maafisa wetu mahakamani kuhakikisha juu ya kesi zao kama watenda makosa lakini mwisho wa siku Sheria inataka iwalinde" amesema.

    Kwa mujibu wa Wizara husika, taasisi za usaidizi wa sheria, waratibu na wadau mbali mbali mbali, suala la usaidizi wa sheria linahitaji kupewa kipaumbele Zaid huku wazazi nao wakitakiwa kusimamia msingi mzima wa malezi Kwa watoto wao ili kupatikana kizazi chenye maadili mazuri.

MWISHO..........0772694778