Na Yassir Mkubwa El Bahsaany
MAMLAKA ya Usafiri Baharini imesema serikali imeridhia kampuni za uwekezaji nchini zinazotoa huduma za usafiri wa Baharini kuongezeka bei za nauli za usafiri kutoka Dar es Salam na Ulnguja kwa daraja la chini kutoka shilingi 30000 hadi 35000 ambazo zilianza kitumika rasmi Oktoba 7 mwaka huu.
Akizungumza na vyombo vya habari katika ofisi za mamlaka hiyo Bandarini Mkirugenzi Mkuu wa Mamlaka hiyo Mtumwa Said, alisema kiridhia kwa ombi hilo kunatokana na hoja zilizowasiahwa na kampuni hizo juu ya ongezeko la nauli katika boti.
Akizitaja hoja zilizowasilishwa na kampuni hizo za usafirishaji alisema ni kuongezeka kwa Bei za gharama za mafuta ambapo kampuni zilieleza kuwa Bei ya nauli kwa tiketi ya shilingi 30,000 kwa daraja la chini ilitangazwa mnamo mwaka 2022 ambapo kwa wakati huyo bei ya mafuta ulikuwa ni shilingi 2500 ikilinganishwa na mwaka huu ambapo Bei ya mafuta ni shilingi 3020 kwa lita.
Alisema ongezeko hilo limepelekea gharama za uendeshaji kuongezeka kwa asilimia 21 na Bei ya tiketi imeendelea kubaki ile ile.
Mkirugenzi Mtumwa alisema hoja nyengine ni kupanda kwa Bei ya fedha ya dola za kimarekani dhidi ya shilingi za kitanzania kwani kikawaida kampuni hizo zimekuwa zikilipa Kodi, kununua vifaa pamoja na kufanya matengenezo ya vyombo vyao kwa kutumia dola badala ya shilingi za kitanzania.
Alifahamisha kuwa mwaka 2022 dola ulikuwa sawa na shilingi za kitanzania 2,330 ambapo mwaka huu dola 1 ni sawa na shilingi 2,850 katika soko la kawaida ambayo hufanya ongezeko la asilimia 22 ya uendeshaji huku kampuni zimekuwa zikilipa Kodi TRA kwa dola badala ya shilingi ya kitanzania jambo linalopelekea pia kuongezeka kwa gharama za uendeshaji.
Hata hivyo sababu nyengine alisema ni gharama za matengenezo na utawala ambapo kampuni zililalamika kuongezeka kwa gharama za utawala na matengenezo ya vyombo kwa kipindi hichi ambapo dola imepanda ikilinganishwa na Bei ya abiria Kama ilivyo kwa kipindi Cha miaka miwili iliyopita.
Alisema serikali ilizijadili hoja hizo pamoja na kizofanyia uchambuzi taarifa zote za kifedha za uendeshaji za kampuni hizo na kubaini kwa kiasi haziendani na Bei halisi iliyokiwa ikitozwa hapo awali ya shilingi 30,000.
"Bei iliyowasilishwa awali na iliyopatikana ilikiwa ni zaidi ya shilingi 35000 iliyokibaliwa hivi sasa, serikali kwa kuzingatia hali za maisha ya wananchi wake hasa wa daraja la chini katika mazungumzo yaliyofanyika tuliwaomba sana wawekezaji/ kampuni hizi kukubali ombi la serikali kufikia shilingi 35000 kwa daraja la chini na kampuni zilitukubalia," alisema.
Hivyo aliwakumbusha wadau wote wa usafirishaji Baharini kuzingatia Bei iliyoidhinishwa na serikali na kufanya tofauti ni kwenda kinyume na Sheria na kampuni za usafiri Baharini na hatua kali za kisheria zitachukuliwa kwa watakaobainika.
Sambamba na hayo aliwasisitiza wananchi kununua tiketi katika ofisi rasmi za kampuni za meli au boti na kuacha kununua tiketi za kusafiria kwa walanguzi na kupelekea kuuziwa kwa Bei za juu.
Mbali na hayo aliwakumbusha wamiliki wa vyombo vya usafiri kuzingatia Sheria, kanuni na miongozo yote inayosimamia usalama katika usafiri wa Baharini ikiweno kupakia abiria kwa mujibu wa uwezo wa chombo kama ilivyoidhinishwa na mamlaka
Aliahidi kuwa mamlaka itaendelea kusimamia jukumu lake kwani ndio mamlaka yenye dhamana ya Usafiri Baharini Zanzibar.
Nao wananchi wanaotumia huduma hzo za usafiri Said Ali Abdalla, Juma Daud Ali na Salma Juma khalfan walisema wamesikitishwa sana na ongezeko hilo la bei kwani wananchi wengi hali zao ni duni na wanafanya shughuli zao za kujitafitia kipato.
Walisema ni vyema serikali kuwaangalia kushushwa kwa bei hiyo kwani tiketi zipandishwa mara kwa mara na wengi wanaosafiri kutoka Unguja kwenda Dar es Salam wanakwenda kwa ajili ya kufanya biashara kujitafutia kipato Cha kuendesha familia zao.
Mwisho