Tuesday, 17 October 2023

WADAU WA KUPINGA VITENDO VYA UDHALILISHAJI WAIJADILI SHERIA YA MTOTO NAMBARI 6 YA MWAKA 2011



Na Yassir Mkubwa EL BAHSAANY

Wadau wa kupinga Vitendo vya Ukatili na Udhalilishaji wa kijinsia wamesema Sheria ya Mtoto namba 6 ya mwaka 2011 ni vyema ikatambua mgawanyo  wa haki za watoto kwa kuzingatia umri ili kulinda maslahi na ustawi wa mtoto.

Wito huo umetolewa na na Hakimu dhamana Mkoa wa Kusini Unguja ndugu Khamis Rashid Khamis  Mara baada ya kikao  cha Mapitio cha  kujadili  sheria ya Mtoto na kutoa maoni kilichofanyika katika ukumbi wa kidongo chekundu Mental.

Amesema ni wakati sahihi  wa kueka sheria ambayo Itatoa muongozo wa kushughulikia watoto wenye umri wa chini ya miaka 14  na 16 na kuweka utaratibu wa kusikiliza kesi zao.





Hata hivyo amependekeza  suala la kueka sheria kwa skuli zinazolea watoto kuhakisha wanaimarisha mfumo wa kuieka saikolijia ya mtoto mhanga wa matukio mbali mbali nchini.

Mkurugenzi Idara ya Maendeleo ya Jamii,Jinsia Wazee  na Watoto ndugu Siti Abas Ali amesema umuhimu wa marekebisho ya Sheria ya  mtoto ni pamoja na maendeleo ya sayansi na teknolojia  ambayo kimsingi yameongeza haja ya kuimarisha baadhi ya vipengele vyake.

Aidha Mkurugenzi Siti amesisitiza suala la ushirikiano na wadau mbali mbali katika katika mapambano ya ukiukwaji wa haki za mtoto.

Amesema Wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto ipo tayari kushirikiana  na wadau hao  ili kufanikisha azma ya kuleta ustawi wa mtoto.

Baadhi ya wanasheria wamesema kikao hicho ni miongoni mwa sheria yoyote ni kutekeleza hivyo uwepo wa Ushirikishwaji wa wadau hao utasaidia kuleta ufanisi wa kiutekekelezaji wa sheria hiyo.

Wizara ya Maendeleo ya jamii jinsia Wazee na watoto inaendelea na ukusanyaji wa maoni ya sheria ya hiyo kwa lengo la kuipata sheria mpya na iweze kudumu kwa muda mrefu.

MWISHO

No comments:

Post a Comment