Thursday, 20 July 2023

FURAHA YA WATOTO IMEONGEZEKA KWA KUPEWA MIKOBA RC AYOUB ASHUHUDIA

 Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Unguja Ayoub Mohamed Mahmoud amesema serikali inaendelea kushirikiana na sekta binafsi ili kuona changamoto zinazozikabili sekta mbalimbali ikiwemo elimu zinapatiwa ufumbuzi.

 Akizungumza katika hafla ya ugawaji wa vifaa  vya elimu kwa wanafunzi wa skuli ya Mgonjoni  vilivyotolewa naTaasisi ya Bhoke Moren Foundation  amesema kutolewa kwa vifaa hivyo vitawasaidia wanafunzi hao kusoma katika mazingira mazuri.

 Amesema matumaini yake kuwa taasisi hiyo inakuwa mkombozi wa wanafunzi ktk sekta ya elimu hapa zanzibar .Amesema serikali imefanya juhudi za kutosha kuhakikisha kijiji cha mgonjon kinapata mafanikio pamoja na kupatiwa huduma zote za msingi ikiwemo elimu na huduma nyengine za kijamii.

 Mwenyekiti wa Bhoke Moroni Foundation Bhoke Moroni amesema taasisi ya Bhoke amelenga kusaidia watoto wenye kuishi katika mazingira magumu hivyo atahakikisha misaada yote inayotolewa inawafikia walengwa ili kuwaondolea changamoto mbalimbali ikiwemo kwenye elimu. Ameeleza lengo ni kuinua ufaulu wa wanafunzi wenye kuishi katika mazingira magumu wakiwemo watoto yatima amesema katika kuangalia mazingira wamegundua mazingira hatarisi ikiwemo viatu na sare za skuli.

Ameahidi kuwapatia wanafunzi viatu na sare za skuli ili kuondoa tatizo hilo ambalo wanafunzi wengi wanakabiliwa nalo kutokana na ugumu wa maisha katika familia zao.

Akisoma Risala ya walimu ya Skuli ya Mgongoni Mwalimu Zainab Sururu Vuai amesema Skuli ya Mgonjon bado inakabiliwa na changamoto  ya Uzio wa skuli, Usafiri kwa walimu, ukosefu wa uwanja wa michezo, walimu wa masomo ya Sayansi komputa na ICT.Hivyo ameiyomba serikali kupitia wizara ya elimu kuongeza bajeti ili kujiendesha kwa ufanisi katika kukuza ufaulu kwa wanafunzi wa skuli hiyo. 

Hata hivyo waliishukuru taasisi ya msaada Bhoke Moroni Foundation kwa kuwapatia msaada hu wa vifaa na kuahidi  kuvitumia kwa lengo lililokusudiwa na taaasisi hiyo. Nao wanafunzi waliokabidhiwa msaada huo wamatoa shukurani zao za dhati kwa taasisi ya Bhoke ambao utawasaidia katika masomo yao. 


Tuesday, 18 July 2023

DKT MWINYI MGENI RASMIN KILELE CHA MAADHIMISHO YA MWAKA MPYA WA KIISLAMU PEMBA

 DK. MWINYI AKAMILISHA ZIARA YAKE PEMBA

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Al hajj. Dk. Hussein Ali Mwinyi amehimiza jamii kuweka mkazo zaidi kwenye malezi ya watoto na vijana ili kukuza taifa lenye maadili, nidhamu na kizazi chema chenye kumjua Mwenyezi Mungu.

Al hajj Dk. Mwinyi aliyasema hayo kwenye kilele cha maadhimisho ya Mwaka mpaya wa Kiislam Zanzibar, 1445 Hijria, masjid  Munawwara, Mfikiwa  Mkoa wa Kusini, Pemba.

Alisema, ni wajibu wa wazazi na walezi kuwasimamia vyema watoto wao na kuwapa elimu ya dini na dunia ili kuwaepusha na vitendo vya uvunjivu wa amani, tabia mbaya na vitendo vya udhalilishaji.

Akizungumzia historia ya tarehe ya Kiislaam, Al hajj Dk. Mwinyi alieleza ilianza mara baada ya  Mtume SAW kuhama Makka na kuhamia Madina ambako utulivu na Amani ulipatikana na kuwa chanzo cha kuenea uislam dunia nzima.

Alisema lengo la kuadhimishwa mwaka Mpya wa Kiislam 1445 H ni kuendelea kusisitiza na kuhimiza amani, ushirikiano na upendo kwenye jamii Katika kutekeleza mambo ya heri.

Aidha, aliendelea kuhimiza Umoja na mshikamano kwenye jamii ili nchi izidi kupata neema na baraka kutoka kwa Mola.

Akizungumza kwenye hafla hiyo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Haroon Ali Suleiman, alipongeza ushirikiano uliopo baina viongozi wa Mkoa wa Kusini na Kaskazini Pemba na viongozi wa Chama, katika kutela Maendeleo ya kisiwa hicho.

Akiwasilisha mada nidhamu ya kodi kwenye kongamano la mwaka mpya wa kiislaam 1445, Sheikh Said Ahmad aliwataka watumishi wa Umma kuutumia vyema muda wa Serikali wanapokua kwenye majukumu yao ili kukwepa kuchuma mali za dhulma zinazotokana na utumishi waa hasa kwenye ibada zao.

Pia alihimiza umuhimu wa kulipa Kodi kwa  serikali kwa mujibu wa sheria za Kiislam.

 Naye Sheikh  Izud Alaw wa Mombasa Kenya,  aliwahimiza waumini wa Kiislam juu ya umuhimu wa kuzingatia vyema tarehe za kiislam kwenye mfumo wa maisha yao.

Pia alieza miezi ya Kiislaam inabeba mfumo mzima wa  maisha ya binaadam.

Vile vile, aliwataka waumini wa dini ya Kiislaam kutofungamana na kufuatilia masuala na muandamo wa mwenzi na hitilafu za Arafa pekee pia waangalie mambo mengine muhimu ikiwemo suala la eda kwa mwanamke alieacha ama kufiliwa na mumewe kwa tarehe zinapoanza hadi kumalizika kwake.

Akiwasilisha taarifa ya maadhimisho ya mwaka mpya wa Kiislam 1445, Katibu Mtendaji wa Ofisi ya Mufti , Sheikh Khalid Mfaume, alisema lengo la maadhimisho hayo ni kuitangaza tarehe ya kiislam na kuendeleza historia ya dini walioiacha maulamaa na kuahidi ofisi ya Mufti inajukimu ya kuendelea kuitangaza na kuishajisha kwa jamii.

Alisema maadhimisho ya mwaka mpya wa Kiislam yalifanikishwa kwa matukio mbalimbali ikiwemo kutoa huduma za macho kwenye hospitali ya kivunge, Mkoa wa Kaskazini Unguja, kusomwa dua ya kuliombea Taifa, kufanikishwa kwa kongamano kuwa la wanawake wa Kiislam lililohudhuriwa na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Hajjat Dk. Samia Suluhu Hassan, maonesho ya kiislam ya biashara yaliyowashirikisha wafanyabiasha wadogo na wajasiriamali, matembezi ya Zafa, kisiwani Pemba  yaliolenga kuboresha afya pamoja na matembezi ya hiari yatafanyika Unguja.

MWISHO.




MAHAKAMA YAMUACHIA HURU AFANDE RAMA

 NA YASSIR MKUBWA EL BAHSAANY

MAHAKAMA YAMUACHIA HURU AFANDE RAMA

Mahkama ya Mkoa wa Vuga mjini Unguja  imemuachua huru mshtakiwa Ramadha Ali ( Afande Rama) aliekua kikabiliwa na kosa la kuruhusu kuingiliwa kuingiliwa.

Mshtakiwa  mwenye kesi namba 59/ 2023 leo ameachiwa huru baada ya hakimu wa mahakama hiyo kudai mshatakiwa hana hatia.

Akitoa hukumu ya kumuachia huru hakimu wa mahakama ya hiyo  Mhe Khamis Ali Simai amesema mshitakiwa hana hatia hvyo amemuachia huru kwa kifungu cha 220 sheria namba 7 ya mwaka 2018.

Kesi hiyo imewasilishwa na muendesha mashitaka kutoka ofisi ya mkurugenzi wa mashtaka Mohd Saleh Jumla ya mashahidi 9 wamewasilisha ushahidi ambao ushahidi wote haukuweza kumtia hatiani mshtakiwa huyo.

Itakumbukwa kuwa Ramadhani alishatakiwa baada ya kusambaa kwa video zilizodhaniwa kuwa ni yeye ambae aliruhusu kuingiliwa wakati akiwa mtumishi wa jeshi la Polisi.

MWISHO.