Tuesday, 18 July 2023

MAHAKAMA YAMUACHIA HURU AFANDE RAMA

 NA YASSIR MKUBWA EL BAHSAANY

MAHAKAMA YAMUACHIA HURU AFANDE RAMA

Mahkama ya Mkoa wa Vuga mjini Unguja  imemuachua huru mshtakiwa Ramadha Ali ( Afande Rama) aliekua kikabiliwa na kosa la kuruhusu kuingiliwa kuingiliwa.

Mshtakiwa  mwenye kesi namba 59/ 2023 leo ameachiwa huru baada ya hakimu wa mahakama hiyo kudai mshatakiwa hana hatia.

Akitoa hukumu ya kumuachia huru hakimu wa mahakama ya hiyo  Mhe Khamis Ali Simai amesema mshitakiwa hana hatia hvyo amemuachia huru kwa kifungu cha 220 sheria namba 7 ya mwaka 2018.

Kesi hiyo imewasilishwa na muendesha mashitaka kutoka ofisi ya mkurugenzi wa mashtaka Mohd Saleh Jumla ya mashahidi 9 wamewasilisha ushahidi ambao ushahidi wote haukuweza kumtia hatiani mshtakiwa huyo.

Itakumbukwa kuwa Ramadhani alishatakiwa baada ya kusambaa kwa video zilizodhaniwa kuwa ni yeye ambae aliruhusu kuingiliwa wakati akiwa mtumishi wa jeshi la Polisi.

MWISHO.


No comments:

Post a Comment