Friday, 1 November 2024

Vita vya Ukraine: Ndege 31 zisizo na rubani zimedunguliwa Ukraine, Jeshi la anga la Ukraine lasema

 Vita vya Ukraine: Ndege 31 zisizo na rubani zimedunguliwa Ukraine, Jeshi la anga la Ukraine lasema

kulingana na ripoti ya kila siku ya Ukraine kuhusu ya jeshi la anga la Ukraine, Usiku wa tarehe 1 Novemba, jeshi la Urusi limeishambulia Ukraine kwa makombora matatu ya ndege ya X-59/69, droni 48 za aina ya Shahed, pamoja na droni za "aina isiyojulikana,".
Pia inabainisha kuwa mfumo wa ulinzi wa anga, ulidungua droni 31 kwa risasi na droni nyingine 14 "zilipotea ndani," na tatu zaidi ziliruka kuelekea Belarus.
"Pia, ulinzi wa anga ulifanikiwa kuangusha kombora moja la ndege iliyokuwa ikiongozwa na droni ya X-59/69. Malengo ya mashambulizi ya Urusi hayakufikiwa,"
ripoti hiyo inasema,Jeshi la anga lilibaini kuwa, hakukuwa na majeruhi.
wizara ya ulinzi ya Urusi imesema,Urusi inaripoti kuwa jana usiku, mifumo ya ulinzi wa anga ilidungua ndege zisizo na rubani 83 za Ukraine katika maeneo ya Kursk, Voronezh, Bryansk, Oryol na Belgorod, pamoja na eneo lililotwaliwa na Urusi.



No comments:

Post a Comment