Sunday, 24 November 2024

TAMWA YATOWA MAFUNZO KWA WAHAMASISHAJI JAMII KUHUSU MAFUNZO YA NAFASI ZA UONGOZI KWA WANAWAKE

 




Na Muandishi wetu.

Katika juhudi za kuimarisha ushiriki wa wanawake katika uongozi na kukuza haki za kidemokrasia, Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania, Zanzibar (TAMWA- ZNZ) kimetoa mafunzo ya siku mbili kwa Wahamasishaji Jamii (Citizen Brigades) wapatao 60 kwa upande wa Unguja ikiwa ni sehemu ya program ya kuimarisha uongozi kwa wanawake (SWIL) wenye lengo la kujenga jamii yenye usawa wa kijinsia kwa kuwawezesha wanawake kushika nafasi katika ngazi za maamuzi.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo, Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano TAMWA ZNZ, Saphia Ngalapi, ameeleza kuwa watekelezaji wa program wanaimani na wahamasishaji waliopatiwa mafunzo na kuwawata kuwa mabingwa wakuhamasisha jamii juu ya haki za wanawake kushiriki katika uongozi.

"Kupitiatimuhii, tunatarajia mabadiliko katika kutoa elimu kwa jamii kuhusu haki ya demokrasia na uongozi kwa wanawake ili kufikia 50% kwa 50% katika ngazi za maamuzi, jambo litakalochangia kuleta maendeleo endelevu kwawote" alisema Ngalapi.

Afisa Ufuatiliaji na Tathmini TAMWA ZNZ, Mohamed Khatib, aliwasisitizia wahamasishaji hao juu ya umuhimu wa kazi yao katika kukuza nafasi za wanawake katika uongozi.

"Tufahamu kuwa hili jambo la kuelimisha jamii si ajira bali ni kazi yakujitolea kuhakikisha matarajio ya wanawake kushika nafasi za uongozi yanafikiwa kwa kubadilisha mitazamo ya jamii, uchaguzi wa 2025, tunataka tuone wanawake wanashika nafasi za uongozi kuanzia ngazi za shina hadi Taifa kwani uwezo huo wanao, alifafanua afisa huyo.





Mafunzo haya yamejumuisha wawakilishi kutoka makundi mbali mbali ya kijamii ikiwemo viongozi wa dini, watu wenye ulemavu, wanaharakati wa kupinga vitendo vya udhalilishaji na wanaume wa mabadiliko.

Nae mkufunzi ni mafunzo hayo ya siku mbili Asha Abdi aliwahimiza wahamasishaji jamii kuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha malengo ya mradi huu yanafikiwa.

Ukhty Amina Salum ambae ni kiongozi wa dini na mwanaharakati wa siku nyingi ameeleza shukrani zake kwa kuchaguliwa kuwa sehemu ya wahamasishaji wa jamii. "Nafurahi kuwa miongoni mwa wahamasishaji wa jamii, dhamana hii nitaibeba na kuhakikisha jamii inahamasika na kuachana na dhana potofu juu ya uwezo wa mwanamke na maamrisho ya dini kuhusiana na wanawake kushiriki katika uongozi alisema Ukhty Amina.

Nae Haji Khamis Haji kutoka Mkoa wa Kaskazini Unguja alisisitiza kuwa elimu aliyoipata itamsaidia kuhamasisha jamii katika mkoa wake kutambua haki zao za kidemokrasia na kuongeza wanawake katika nafasi za uongozi.

Mafunzo haya yanaashiria jitihada za TAMWA- ZNZ kwa kushirikiana na Jumuiya ya Wanawake Wenye Ulemavu Zanzibar (JUWAUZA), Jumuiya ya Mazingira, Jinsia na Utetezi Pemba (PEGAO) Jumuiya ya Wanasheria Wanawake Zanzibar (ZAFELA) kwa mashirikiano makubwana Ubalozi wa Norway katika kuwaandaa wanawake wenye nia ya kugombea nafasi za uongozi kuelekea uchaguzi wa 2025, huku wakilenga kuongeza idadi ya wanawake katika ngazi za maamuzi visiwani Zanzibar.










Saturday, 23 November 2024

WANANCHI WAPIMWA AFYA ZAO BURE KUELEKEA KATIKA MAADHIMISHO YA WIKI YA UVUVI

 




Na Seif Mbarouk - Malindi

Wavuvi mbali mbali wametakiwa kuunga mkono shamrashamra za wiki ya uvuvi katika ukataji wa leseni za uvuvi ili kuachana na uvuvi haramu unaoendelea kufanyika siku hadi siku.

Amesema hayo Meneja wa Diko na Soko la Samaki la Malindi Nd. Mohd Idarus Mohd wakati wa ufanyaji wa usafi wa soko la samaki pamoja na upimaji wa afya kwa wananchi huko Malindi Mkoa wa Mjini Unguja.

Meneja huyo amesema miongoni mwa shamrashamra za wiki ya mvuvi ni kuwahamasisha wavuvi kufuata sharia za uvuvi ikiwemo ukataji wa leseni kwa ajili ya kuimarisha shughuli za uchumi wa buluu nchini.

Sambamba na hayo amesema lengo la kuadhimisha siku ya Mvuvi Duniani nu kujadili mambo mbali mbali yanayohusiana na uvuvi ili kutambua umuhimu wa sekta ya uvuvi pamoja na kutatua changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta hiyo.

Kwa upande wake Mratibu wa Kifua Kikuu Zanzibar Dkt. Rahma Omar kutoka Shirika la Amred Tanzania amesema lengo la kuendesha shughuli za afya katika Soko la Malindi ni kuwasogezea huduma kwa karibu ili kuwakinga na hatari ya kupata ugonjwa wa kifua kikuu.

Vilevile amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imegharamia huduma za afya kwa wananchi hivyo wananchi mbalimbali wanapaswa kujitokeza kwa wingi kupata huduma mbalimbali kama upimaji wa shindikizo la damu ,homa ya ini ,kisukari na mengineo.

Kwa upande wao Washiriki wa zoezi hilo wamesema wameishukuru Serikali kwa kuadhimisha siku ya Mvuvi Duniani kwa kuwaletea huduma ya afya bure na kutoa wito kwa wavuvi wa diko la Malindi kuja kushiriki zoezi hili ili kuwa na uhakika wa afya zao.

MWISHO.


Wednesday, 20 November 2024

MTU MMOJA MIKONONI MWA POLISI AKITUHUMIWA KUBAKA NA KUSABABISHA KIFO CHA MTOTO WA MIAKA SITA

 MTU MMOJA MIKONONI MWA POLISI AKITUHUMIWA KUBAKA NA KUSABABISHA KIFO CHA MTOTO WA MIAKA SITA





Jeshi la Polisi Mkoa wa Kusini Unguja linamshikilia mtu mmoja aitwae Maulid Hassan Maulid (18) mkaazi wa Mwera Pongwe katika Wilaya ya Kati, Mkoa wa Kusini Unguja kwa tuhuma za mauaji ya mtoto mdogo Khadija Dadi Mhoda (06) mwanafunzi wa chekechea mkaazi wa Mwera Vichaka mabundi, shehia ya ubago.
Akizungumza na waandishi wa habari huko Tunguu , Makao Makuu ya Polisi Mkoa wa Kusini unguja, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Daniel Shillah amesema tukio hilo la Mauaji lilitokea Novemba 14, 2024 huko Mwera Vichaka Mabundi ambapo Mtuhumiwa huyo alimwingilia kimwili na kumsababishia kifo chake.
Kamanda SHILLAH amesema Jeshi la Polisi Katika Mkoa huo linaendelea kufanya upelelezi ili mtuhumiwa huyo afikishwe Mahakamani.

AJALI ZINAWEZA KUEPUKIKA KWA MADEREVA IKIWA WATAKWENDA MWENDO WA WASTANI


Na Muandishi wetu

Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Unguja, Rashid Hadid Rashid, amewataka madereva kwenda mwendo wa wastani wakati wanapoendesha vyombo vya moto ili kuepuka ajali zisizo za lazima.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu huyo, wakati akifungua mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kuendesha kwa usalama, madereva na makonda wa gari za abiria wa mkoa huo, katika ukumbi wa Ofisi ya Polisi Mkoa wa Kaskazini Unguja, Mkuu wa Wilaya ya Kaskazini ‘B’, Othman Ali Maulid, amesema uzowefu unaonesha kuwa mwendo kasi unachangia ajali nyingi za barabarani na kuwataka wadau hao kufuata maelekezo ya mwendo yaliyowekwa katika alama za barabarani ili watumiaji wa barabara wabaki kuwa salama.
Ameeleza kuwa Serikali imeweka miundombinu ya barabara ili kuhakikisha sekta ya usafiri nchini inaimarika na kuwasihi kuitumia miundombinu hiyo kama ilivyokusudiwa pasi na kuathiri watumiaji.
"Tunapoendesha vyombo vyetu kwa mwendo wa wastani itasaidia kupunguza ajali na endapo zitatokea hzaitakua kubwa kama itavyokua ajali ya mwendo kasi.” alisema Mkuu huyo.
Aidha amewataka waliopatiwa mafunzo hayo kuwa mabalozi wazuri wa elimu hiyo ili kuiweka Zanzibar katika hali ya usalama kutokana na ajali za barabarani kwa Zanzibar bila ya ajali inawezekana.
Naye Mkuu wa Kituo cha Umahiri cha Kikanda katika Usalama Barabarani, Chuo Cha Taifa Cha Usafishaji (NIT ), Godlisten Msomanje amesema lengo la mafunzo hayo ni kuhamasisha matumizi salama ya barabara katika kuadhimisha wiki ya usalama barabarani.
Alieleza kuwa chuo hicho kinatoa mafunzo kwa madereva, kufanya utafiti na kutoa ushauri elekezi ili kuhakikisha usalama wa wananchi barabarani unakuwepo muda wote.
Amesema uzowefu unaonesha kuwa tatizo la usalama barabarani ni janga la kitaifa hivyo elimu inahitajika zaidi ili kuondoa tatizo hilo
“tumekuja Zanzibar kutoa elimu dhidi ya usalama barabarani ili kusaidia kuweka usalama wa watumiaji wa barabara.” Alisema mkuu huyo
Akiwasilisha mada ya Sheria na alama za barabarani, Mhandisi Mhonja Roheje, amesema madereva wengi wanaenda kinyume na taratibu na sharia za barabarani ikiwa ni pamoja na kuendesha bila kuwa na leseni ya udereva, kutokagua vyombo vyao kabla ya kuingia barabarani pamoja na kutofuata alama za barabarani.
“Iwapo utakua na leseni lakini unajaza abiria kupitia kiasi bado hujafuata sheria jambo ambalo linahatarisha usalama wa abiria na watumiaji wengine wa barabara na kuiomba Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kusimamia mikakati zaidi ili kukomesha tabia za madereva na makonda wanaofanya makosa hayo.”alisema Mhandisi huyo
Kwa upande wa madereva na makondawaliyopatiwa mafunzo hayo wameahidi kuyafanyia kazi kwa maslahi ya watumiai wa barabara na Taifa kwa ujumla na kuziomba taasisi husika kuwapatia mafunzo ya mara kwa mara ili kutekeleza majukuumu yao kwa ufanisi.
Mafunzo hayo yametolewa na Mamlaka ya Usalama Barabarani Zanzibar kwa kushirikiana na Chuo Cha Usafirishaji Tanzania, ikiwa ni shamrashamra za wiki ya nenda kwa usalama Barabarani.








Friday, 1 November 2024

Vita vya Ukraine: Ndege 31 zisizo na rubani zimedunguliwa Ukraine, Jeshi la anga la Ukraine lasema

 Vita vya Ukraine: Ndege 31 zisizo na rubani zimedunguliwa Ukraine, Jeshi la anga la Ukraine lasema

kulingana na ripoti ya kila siku ya Ukraine kuhusu ya jeshi la anga la Ukraine, Usiku wa tarehe 1 Novemba, jeshi la Urusi limeishambulia Ukraine kwa makombora matatu ya ndege ya X-59/69, droni 48 za aina ya Shahed, pamoja na droni za "aina isiyojulikana,".
Pia inabainisha kuwa mfumo wa ulinzi wa anga, ulidungua droni 31 kwa risasi na droni nyingine 14 "zilipotea ndani," na tatu zaidi ziliruka kuelekea Belarus.
"Pia, ulinzi wa anga ulifanikiwa kuangusha kombora moja la ndege iliyokuwa ikiongozwa na droni ya X-59/69. Malengo ya mashambulizi ya Urusi hayakufikiwa,"
ripoti hiyo inasema,Jeshi la anga lilibaini kuwa, hakukuwa na majeruhi.
wizara ya ulinzi ya Urusi imesema,Urusi inaripoti kuwa jana usiku, mifumo ya ulinzi wa anga ilidungua ndege zisizo na rubani 83 za Ukraine katika maeneo ya Kursk, Voronezh, Bryansk, Oryol na Belgorod, pamoja na eneo lililotwaliwa na Urusi.



Uhispania yaomboleza huku idadi ya vifo vya watu waliofariki kutokana na mafuriko ikizidi 150

 Uhispania yaomboleza huku idadi ya vifo vya watu waliofariki kutokana na mafuriko ikizidi 150

Takriban watu 158 wamefariki katika maafa makubwa zaidi ya mafuriko nchini Uhispania katika vizazi huku waokoaji wakipambana kutafuta manusura.
Siku ya Alhamisi zaidi ya wafanyakazi 1,200, wakisaidiwa na ndege zisizo na rubani, wametumwa kufanya kazi ya uokoaji huku mvua ikiendelea kusababisha tisho la maafa zaidi maeneo mbali mbali ya nchi hiyo.
Lakini katika baadhi ya miji iliyoathiriwa zaidi na mafuriko ya Jumanne usiku, watu walikumbwa na kazi ya kuopoa miili kutoka kwenye matope na vifusi vya majengo yaliyoporomoka kufuatia mafuriko.
Vifo visivyopungua 155 vilirekodiwa katika mji wa Valencia, huku vingine viwili vikirekodiwa katika eneo la Castilla-La Mancha magharibi mwa jimbo hilo, na raia Muingereza, ametangazwa kufariki Andalusia.



Sunday, 13 October 2024

ZMA YARIDHIA ONGEZEKO LA BEI YA NAULI ZA BOTI WASAFIRI WALALAMIKIA HALI


Na  Yassir Mkubwa El Bahsaany

 MAMLAKA ya Usafiri Baharini imesema serikali imeridhia kampuni za uwekezaji nchini zinazotoa huduma za usafiri wa Baharini kuongezeka bei za nauli za usafiri kutoka Dar es Salam na Ulnguja  kwa daraja la chini kutoka shilingi 30000 hadi 35000 ambazo zilianza kitumika rasmi Oktoba 7 mwaka huu.

Akizungumza na vyombo vya habari katika ofisi za mamlaka hiyo Bandarini  Mkirugenzi Mkuu wa Mamlaka hiyo Mtumwa Said, alisema kiridhia kwa ombi hilo kunatokana na hoja zilizowasiahwa na kampuni hizo juu ya ongezeko la nauli katika boti.

Akizitaja hoja zilizowasilishwa na kampuni hizo za usafirishaji alisema ni kuongezeka kwa Bei za gharama za mafuta ambapo kampuni zilieleza kuwa Bei ya nauli kwa tiketi ya shilingi 30,000 kwa daraja la chini ilitangazwa mnamo mwaka 2022 ambapo kwa wakati huyo bei  ya mafuta ulikuwa ni shilingi 2500 ikilinganishwa na mwaka huu ambapo Bei ya mafuta ni shilingi 3020 kwa lita.

Alisema ongezeko hilo limepelekea gharama za uendeshaji kuongezeka kwa asilimia 21 na Bei ya tiketi imeendelea kubaki ile ile.

Mkirugenzi Mtumwa alisema hoja nyengine ni kupanda kwa Bei ya fedha ya dola za kimarekani dhidi ya shilingi za kitanzania kwani kikawaida kampuni hizo zimekuwa zikilipa Kodi, kununua vifaa pamoja na kufanya matengenezo ya vyombo vyao kwa kutumia dola badala ya shilingi za kitanzania.

Alifahamisha kuwa mwaka 2022 dola ulikuwa sawa na shilingi za kitanzania 2,330 ambapo mwaka huu dola 1 ni sawa na shilingi 2,850 katika soko la kawaida ambayo hufanya ongezeko la asilimia 22 ya uendeshaji huku kampuni zimekuwa zikilipa Kodi TRA kwa dola badala ya shilingi ya kitanzania jambo linalopelekea pia kuongezeka kwa gharama za uendeshaji.

Hata hivyo sababu nyengine alisema ni gharama za matengenezo na utawala ambapo kampuni zililalamika kuongezeka kwa gharama za utawala na matengenezo ya vyombo kwa kipindi hichi ambapo dola imepanda ikilinganishwa na Bei ya abiria Kama ilivyo kwa kipindi Cha miaka miwili iliyopita.

Alisema serikali ilizijadili hoja hizo pamoja na kizofanyia uchambuzi taarifa zote za kifedha za uendeshaji za kampuni hizo na kubaini kwa kiasi haziendani na Bei halisi iliyokiwa ikitozwa hapo awali ya shilingi 30,000.

"Bei iliyowasilishwa awali na iliyopatikana ilikiwa ni zaidi ya shilingi 35000 iliyokibaliwa hivi sasa, serikali kwa kuzingatia hali za maisha ya wananchi wake hasa wa daraja la chini katika mazungumzo yaliyofanyika tuliwaomba sana wawekezaji/ kampuni hizi kukubali ombi la serikali kufikia shilingi 35000 kwa daraja la chini na kampuni zilitukubalia," alisema.

Hivyo aliwakumbusha wadau wote wa usafirishaji Baharini kuzingatia Bei iliyoidhinishwa na serikali na kufanya tofauti ni kwenda kinyume na Sheria na kampuni za usafiri Baharini na hatua kali za kisheria  zitachukuliwa kwa watakaobainika.

Sambamba na hayo aliwasisitiza wananchi kununua tiketi katika ofisi rasmi za kampuni za meli au boti na kuacha kununua tiketi za kusafiria kwa walanguzi na kupelekea kuuziwa kwa Bei za juu.

Mbali na hayo aliwakumbusha wamiliki wa vyombo vya usafiri kuzingatia Sheria, kanuni na miongozo yote inayosimamia usalama katika usafiri wa Baharini ikiweno kupakia abiria kwa mujibu wa uwezo wa chombo kama ilivyoidhinishwa na mamlaka 

Aliahidi kuwa mamlaka itaendelea kusimamia jukumu lake kwani ndio mamlaka yenye dhamana ya Usafiri Baharini Zanzibar.

Nao wananchi wanaotumia huduma hzo za usafiri Said Ali Abdalla, Juma Daud Ali na Salma Juma khalfan walisema  wamesikitishwa sana na  ongezeko hilo la bei kwani wananchi wengi hali zao ni duni na wanafanya shughuli zao za kujitafitia kipato.

Walisema ni vyema serikali kuwaangalia kushushwa kwa bei hiyo kwani tiketi  zipandishwa mara kwa mara na wengi wanaosafiri kutoka Unguja kwenda Dar es Salam wanakwenda kwa ajili ya kufanya biashara kujitafutia kipato Cha kuendesha familia zao.


Mwisho




Wednesday, 2 October 2024

 TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi katika kuhakikisha kwamba inaenda sambamba na mabadiliko ya teknolojia ikiwa ni pamoja na kurahisisha zoezi la uboreshaji wa daftari la wapiga kura, imeboresha mfumo wa uandikishaji ambao kwa mara ya kwanza utamuwezesha mpiga kura aliyepo kwenye daftari kuazisha mchakato wa kuboresha taarifa zake kwa kutumia simu ya kiganjani au komputa.

Hayo yalisemwa na Mjumbe wa Tume hiyo ambae pia ni Jaji wa Mahakama kuu Asina Abdallah Omar wakari akifunguwa mkutano wa tume hiyo kwa wadau wa uchaguzi katika ukumbi wa Sheikh Idrisa Abdulwakil Kikwajuni Mjini Zanzibar.

Jaji Asina alisema wanaotumia simu za viswaswadu nao hawakuachwa nyuma wanaweza kutumia huduma hiyo na kupata maelekezo pamoja na taarifa zao.

Alisema mzunguko wa sita wa uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura unatarajiwa kuanza Oktoba saba mwaka huu na kukamilika Oktoba 13 mwaka huu kwa visiwa vya Unguja na Pemba.

“Uboreshaji huu kama ilivyokuwa uboreshaji wa mwaka 2015 na 2020 utahusisha matumizi ya teknolojia ya biometric votes registration (BVR) ambapo mfumo huu hutumika katika kumtambua mtu na kumtofautisha na mwingine kwa kuwa unahusisha uchukuaji wa alama za vidole vya mikono, picha na saini na kuhifadhiwa kwenye kanzidata ya wapiga kura”alisema Jjai Asina.

Alisema uboreshaji huo ni tofauti na wa mwaka 2015/2020 ambapo ubereshaji wa mwaka huu utatumia teknolojia ya BVR Kits zilizoboreshwa kwa kuwekewa program endeshi ya kisasa zaidi na pia BVR zitakazotumika zimepunguwa uzito ambapo zitakuwa rahisi kubebeka na kufanya zoezi la ubereshaji wa daftari kuwa rahisi haswa kwenye maeneo ya vijijini na watendaji hulazimika kubeba vifaa kwa umabali mrefu.

Aidha alisema kujiandikisha kuwa mpiga kura zaidi ya mara moja ni kosa la kisheria kwa kuzingatia masharti ya kifungu cha 114(1) cha sheria ya uchaguzi wa Rais, wabunge na madiwani namba moja ya mwaka 2024.

Alisema kifungo hicho kinaeleza kuwa mtu yoyote atakayeomba kuandikishwa zaidi ya mara moja atakuwa ametenda kosa la kisheria na akituwa hatiani adhabu yake ni faini isiyopunguwa kiasi cha shilingi 10,0000 na isiyozidi shilingi 30,0000 au kutumikia kifungo kwa kipindi kisichopunguwa miezi sita na kisichozidi miaka miwili gerezani au vyote kwa pamoja kulipa faini na kifungo gerezani.

“Natumia fursa hii kuwaasa wananchi kujiepusha na kosa la kujiandikisha zaidi ya mara moja na niwaombe wadau mkawaelimishe wananchi kwamba wakajiandikishe mara moja na kwenye kituo kimoja ili kuepuka uvunjaji wa sheria”alisema mjumbe huyo wa Tume.

Hata hivyo alisema Tume imeweka utaratibu kwa watu wenyeulemavu, wazee, wagonjwa, wajawazito na akinamama wenye watoto wachanga watakaokwenda nao vituoni kupewa fursa ya kuhudumiwa bila kupanga foleni lakini zoezi hilo la ubereshaji la daftari la wapiga kura halitawahusu wapiga kura wenye kazi za tume, hawajahama kutoka eneo moja la uchaguzi kwenda eneo jingine au kuboresha taarifa zao.

Aliwataka wadau wa uchaguzi kuwafahamisha wananchi wenye sifa kujitokeza kwa wingi kujiandikisha au koboresha taarifa zao vituoni kwa kuwa utaratibu mzuri wa kuwahudumia umewekwa.

Akiwasilisha mada ya uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura, mwakilishi wa Mkurugenzi wa uchaguzi wa Tume hiyo huru ya Taifa Kailima Ramadhani, alisema zoezi la uboreshaji nchi nzima linatarajiwa kukamilika Machi mwakani ambapo litahusisha mambo mbalimbali ikiwemo kutoa kadi mpya kwa wapigak ura waliopoteza kadi au kadi kuharibika,kuondoa wapiga kura waliokosa sifa kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kuukana uraia wa Tanzania na kifo.

Aliwataja ambao hawana sifa ya kuandikishwa katika daftari la wapiga kura ni mtu aliopo chini ya kiapo cha utii wa nchi nyingine tofauti na Tanzania,amewekwa kizuwizini kama mhalifu mwenye ugonjwa wa hana akili, amewekwa kizuwizini kwa ridhaa ya Rais, ametiwa hatiyani kwa kosa ambalo adhabu yake ni kifo na anaetumikia kifungo kwa kosa ambalo adhabu yake inazidi miezi sita iliyotolewa na Mahakama.

Aidha alisema wapiga kura 5,586,433 wapya wanatarajiwa kuandikishwa sawa na asilimia 18.7 ya wapiga kura 29,754,699 waliopo kwenye daftari baada ya uboreshaji uliofanyika mwaka 2019/2020 na wapiga kura 4,369,531 inatarajiwa watabresha taarifa zao.

“Wapiga kura 594,494 inatarajiwa wataondolewa kwenye daftari hivyo baada ya uboreshaji, inatarajiwa kuwa daftari litakuwa na jumla wa wapiga kura 34,746,638”alisema Mkurugenzi huyo.

Wakizungumza katika mkutano huo wadau wa uchaguzi walioshiriki mkutano huo, walisema kuwa zoezi hilo la uboreshaji ni muhimu ambapo wananchi watapata haki yao ya kuandikishwa na kupiga kura katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.











Wednesday, 24 April 2024

DKT MWINYI AMESHIRIKI KATIKA HAULI YA BIN SUMEIT - ASISITIZA UMOJA NA MSHIKAMANO


NA MUANDISHI WETU

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi amehudhuria katika Hafla ya Hauli ya kumuombea dua Alhabib Sheikh Ahmad bin Aboubakar bin Sumeit anaetimiza miaka 102 tokea kufariki kwake.


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi amewaomba wananchi kuendelea kushikamana, kuwa wamoja, kudumisha amani na utulivu ili kuzidi kupiga hatua ya maendeleo ya uchumi na ustawi wa jamii nchini.


Rais Dk.Mwinyi amesema hayo alipojumuika na Waumini wa Dini ya Kiislamu katika Dua ya kumuombea Mwanachuoni mkubwa Zanzibar Alhabyb Ahmad Bin Abuubakar Bin Sumeit iliyofanyika Msikiti wa Ijumaa Malindi , Wilaya ya Mjini Mkoa wa Mjini Magharibi tarehe 22 Aprili 2024.
Rais Dk.Mwinyi ameeleza kuwa leo imemitimia miaka 102 tangu kufariki kwa Mwanachuoni Alhabyb Ahmad Bin Abuubakar Bin Sumeit amemuombea kwa Mwenyezi Mungu amrehemu na Wanazuoni wengine.


Halikadhalika Rais Dk.Mwinyi ameishukuru na kuipongeza Ofisi ya Mufti Mkuu wa Zanzibar kwa kuendelea kuratibu shughuli za Dini na kuzisimamia.
Kwa upande mwingine Rais Dk.Mwinyi amesema jukumu la kuwaombea Dua Waislamu waliotangulia ni la kila Muumini wa Dini hiyo.



Katibu Mtendaji wa Ofisi ya Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Khalid Ali Mfaume na Sheikh Mudhihiriddiyn Ally Qulateyn wakamuelezea Sheikh Alhabib Ahmad bin Aboubakar bin Sumeit katika harakati zake za dini na mazingira ya kuishi na jamii
Hauli hio ya Sheikh Ahmad bin Sumeit imeandaliwa kwa pamoja baina ya uongozi wa Msikiti Gofu na Msikiti Mkuu wa Ijumaa Malindi.

MWISHO.





RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI DKT HUSSEIN ALI MWINYI AMESIMAMA MBELE YA KABURI LA MWANACHUONI MKUBWA AFRIKA MASHARIKI AL HABIB AHMAD BIN ABUBAKAR BIN SUMEIT 
KABURI HILO LIPO MBELE YA MSIKITI WA IJUMAA MALINDI ALIPOSHIRIKI KATIKA HAULI YA KUTIMIZA MIAKA 102 TOKEA KUFARIKI KWAKE.




Thursday, 14 December 2023

VIJANA WA KIKE WAFUZU MAFUNZO YA URENJA NA KULINDA MAZINGIRA YA BAHARI

 

Na YASSIR MKUBWA EL BAHSAANY

Vijana wa kike nchini wametakiwa kuchangamkia fursa zinazotolewa na sekta binafsi ambazo zitawasaidia kuwapatia fursa za kiuchumi pamoja na kujiendeleza kimaendeleo.

Hayo yameelezwa na Mhifadhi wa mazingira ya bahari kisiwa cha chumbe Khamis Khalfan katika sherehe ya kuwapongeza wahitimu wa mafunzo ya urenja huko katika kituo cha walimu kiembe samaki wilaya ya magharibi B mkoa wa mjini magharibi Unguja

Amesema vijana wana nafasi ya kushiriki katika mambo mbali mbali yanayohusu uhifadhi wa mazingira hasa ya bahari ndipo uongozi wa chumbe ukaamuwa kutangaza nafasi kwa vijana ambao watataka kushiriki kwenye mafunzo hayo ya uhifadhi wa bahari

Aidha ameeleza kuwa vijana ambao wamepata nafasi ya kushiriki mafunzo hayo wanarajia kuwa marenja wazuri baada ya kumaliza mafunzo yao ikiwemo kutowa elimu kwa jamii juu ya kutunza mazingira ya bahari na viumbe vya baharini

Kwa upande wake Salim Abdallah Salim kutoka  Kitengo cha Uhifadhi na elimu  chumbe Island amewapongeza vijana hao kwa nafasi walioipata ya ushiriki wa mafunzo ya urenja hivyo amewataka kuendeleza elimu walioipata ya uhifdhi wa mazingira pamoja na kuwapatia vijana wengine.



MSHIRIKI WA MAFUNZO YA URENJA AKIPATIWA CHETI CAKE CHA USHIRIKI KATIKA MAFUNZO YA UHIFADHI WA BAHARI YALIOANDALIWA NA CHUMBE ISLAND


Aidha amesema chumbe island inatowa mafunzo ya uhifadhi wa mazingira kwa vijana mbali mbali pamoja na kuwafundisha namna ya kuogelea na kufanya doria za bahari.

Pamoja na hayo amefahamisha kuwa chumbe island wanaendelea na utwaji wa elimu kwa watu mbali mbali na kuwataka vijana wachangamkie fursa ambazo zinatolewa hapoo

Msimaizi wa urenja kwa upande wa wanawake bi Magret Msemakweli Ntongwa amewahimiza vijana wa kike kujitokeza kwa wingi kwenye mafunzo ambayo yanatulewa chumbe katika nafasi ya urenja hivyo amewataka wale ambao wamepatiwa nafasi hiyo kuwashajihisha wengine kujitokeza pale ambapo nafasi zitatolewa.



MSHIRIKI WA MAFUNZO YA URENJA AKIPATIWA CHETI CAKE CHA USHIRIKI KATIKA MAFUNZO YA UHIFADHI WA BAHARI YALIOANDALIWA NA CHUMBE ISLAND

Nao washiriki wa mafunzo ya urenja wametowa pongezi kwa chumbe island kwa kuona ipo haja kwa vijana wa kike kupewa nafasi ya kushiriki katika uhifadhi wa mazingira na rasilimali za bahari kutokana na nafasi hizo kushikiliwa na wanawake

Jumla ya vijana kumi wa kike wamepatiwa mafunzo ya urenja pamoja na uhifadhi wa mazingira ya bahari pamoja na matumbawe na kufanya doria za usalama bahari na kupatiwa vyeti vya ushiriki pamoja na vijana wawili kupata nafasi ya kuendelea kujifunza zaid kwa muda wa miezi mitatu.

MWISHO.

Thursday, 23 November 2023

VODACOM TANZANIA WATOA BIMA KWA WATOTO 100 MNAZI MMOJA


NA YASSIR MKUBWA - ZANZIBAR TODAY

JUMLA ya mama 100 na watoto 100 wamepatiwa bima kubwa ya bure ya mwaka mzima na kampuni ya Teknologia na mawasiliano Vodadom Tanzania. 

Kina mama hao ni wale waliojifungua watoto wao kunazia Novemba 9 mwaka huu katika hospitali ya Rufaa Mnaznimmoja kupatiwa zawadi hiyo ya upendo. 

Akizungumza katika hafla ya kukabidhi bima hizo Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano Vodacom Tanzania, Anet Kanora, alisema hatua hiyo ni muendelezo wa kampuni hiyo kutoa zawadi kwa wateja wake ikiwa ni njia ya kuwashukuru lakini kwa mwaka huu wameona ipo haja ya kuifikia jamii pana ya watanzania.

Alisema afya ya mama na mtoto ni muhimu kwa kampuni hiyo hivyo wameona ipo haja ya kumpatia bima kubwa mama pamoja na mtoto wake itakayomuwezesha mama na mtoto wake kupata matibabu.

Aidha alisema kwa Tanzania nzima bima hiyo itanufaisha watoto 1000 na mama 1000 lakini kwa Zanzibar kinamama 100 na watoto 100 watanufaika na bima hiyo ya afya.
Alisema bima hizo zitatumika katika hospitali mbalimbali za Zanzibar ikiwemo Ampola Global, Tawakal, Alrahma na hospitali ya Rufaa Mnazimmoja kwa Zanzibar na hospitali ya Muimbili na nyengine za Tanzania bara.   

Mkuu Anet alibainisha kuwa bima hiyo itakuwa haina upendeleo kwani ni lazima watoto wote watakaozaliwa katika kipindi hichi basi wote watanufaika na bima hiyo kuona wanatibiwa magonjwa mbalimbali ikiwemo ya kulazwa ama kutibiwa na kuondoka.
Alibainisha kuwa anaamini bima hiyo itakwenda kuwasaidia wazazi na watoto wao kwani mwaka wa kwanza wa mtoto ni muhimu sana katika upimaji na upatikanaji wa afya bora katika makuzi ya mtoto.

Akizungumzia kuhusu kampeni ya ‘Sambaza Shangwe, Gusa Maisha’ Meneja Mauzo Vodacom Zanzibar, Fadhili Linga, alisema kampeni hiyo ina sehemu mbili, kwanza kuwazawadia wateja kwa zawadi mbalimbali na pili kujikita katika shughuli za kijamii.
Linga alisema sekta ya afya ni eneo muhimu na kampuni hiyo imeona iendeleze jitihada za kuunga mkono serikali kupitia miradi mbalimbali.

Aliahidi kuwa watanendeleza ushirikiano huo ili kuhakikisha upatikanaji wa huduma bora za matibabu ya afya kwa Watanzania wote zinapatikana bila ya usumbufu.
Alisema mbali na kutoa bima pia Vodacom imekuwa ikiwazawadia zawadi kama vile bodaboda, TV, simu za mkononi, router za 4G na 5G na pesa taslimu kuanzia shilingi 500,000 mpaka milioni 10,000,000.

Khadija Salum Said ni Mkuu wa Wodi ya Wazazi hospitali ya Rufaa Mmnazimmoja, aliipongeza kampuni hiyo kwa ubunifu wa kampeni hiyo ambayo inawajali kinamama wanaoleta viumbe wapya duniani.

Alisema kupatiwa bima hizo itasaidia kwa kiasi kikubwa kupatikana kwa huduma ya uhakika ya afya katika hatua ya awali ya watoto wachanga na akina mama waliotoka kujifungua na kupunguza vifo vya mama na watoto wachanga. 

Kwa kupatia bima ya afya ya bure, tena ile kubwa kwa mwaka mzima, akina mama hawa na watoto wao hawatokuwa na shaka pindi watakapokumbwa na changamoto za kiafya, ujio wenu huu umetusaidia sana kupunguza matatizo ambayo yatatokea baada ya mama kujifungua na hata kupunguza vifo vya watoto wachanga,”alisema.

Hivyo, aliiomba kampuni hiyo kuendelea kushirikiana pamoja katika mapambano ya kupunguza vifo vya mama na mtoto kwa kusaidia bima hiyo kwa wazazi wa Tanzania nzima kwani utoaji wa bima hiyo ni njia moja ya kupunguza vifo hivyo. 

Wakizungumza kwa niaba ya wazazi wenzao waliopatiwa bima hizo Maryam Yohana Daniel na Badria Mohammed Khamis aliejifungua watoto mapacha walipongeza Vodacom kwa kuwapatia bima hizo ambazo zitawasaidia kupata matibabu wao na watoto wao na huduma nyengine za kiafya.

Hivyo waliiomba jamii kujiunga na kampuni ya Vodacom ili iweze kusaidia kundi kubwa zaidi katika jamii ya watanzania. 

VodaBima itawawezesha akina mama na watoto wao kupata huduma za afya ni sehemu ya kampeni inayoendelea ya kampuni hiyo nchini kote ijulikanayo kama ‘Sambaza Shangwe, Gusa Maisha’.

MWISHO.




Tuesday, 21 November 2023

MSAADA WA KISHERIA WAWAOKOA WATOTO WANAOKINZANA NA SHERIA ZANZIBAR:

Na AMINA MCHEZO:

   Msaada wa watoto kisheria, kisera na kimipango ni uwanja mpana huku ikionekana sheria iliopo Sasa ya mtoto sheria namba 6 ya mwaka 2011 inamapungufu hivyo wizara ya Màendeleo ya jamií, jinsia, wazee na watoto Zanzibar inafanya juhudi kuhakikisha sheria hiyo inapitiwa upya.

   Sheria hiyo Kwa Sasa inaonekana bado haitoi ulinzi Bora Kwa mtoto hivyo Kwa Sasa wadau na taasisi za usimamizi wa mtoto wamekuwa wakiisindikiza tume ya marekebisho ya sheria ili kuwe na sheria mpya.
 
    "Kwa Sasa tumeshatoka kwenye hatua nyingi za ukusanyaji wa maoni ya wadau na Sasa nadhani tupo katika hatua ya kuishirikisha tume ya marekebisho ya sheria ili tuone kwamba tunapata baraka za mwisho na kunipeleka mbele ili tuwe na sheria mpya ili mambo yawe mazur Kwa watoto" Amesema mkuu wa wa Division  ya hifadhi ya mtoto kupitia idara ya ustawi wa jamii na wazee.

   Mtoto anaekinzana na sheria ni mtoto yeyote alie chini ya umri wa miaka 18 ambae amefanya makosa ya kijinai ikiwemo kubaka, kulawiti, wizi na makosa mengine.
 
  Utafiti umebaini kuwa watoto wengi wanaokinzana na Sheria ni wale watoto wa mzazi mmoja, ndoa kuvunjika, Kukosa matunzo Kwa wazazi wake, hivyo watoto hao hupelekea kuathirika kiakili Kwa kujiingiza katika  makundi maovu na kufanya makosa ya kijinai.

   Kiuhalisia kutokana na sababu hizo inaonekana wazi watoto wanaokinzana na sheria wengi wao ni wale waliopitia udhalilishaji Kwa namna Moja au nyengine kutokana na Kukosa malezi sahihi na Kukosa haki zake za msingi kama mtoto.

    Msaada wa kisheria Kwa watoto wanaokinzana na sheria umeibua hisia tofauti Kwa wanajamii hasa pale wanapoona makosa ya namna hiyo yakijirudia Kila mara
     
     Wengine wanasema kupatiwa msaada wa kisheria ni sawa tu kwani wale ni watoto mengi wanayafanya Kwa kutokujua.
   
     Huku mitazamo ya wengine yakionekana kubeba hisia Kali na kukataa kabisa watoto wale kupewa msaada wakidai kuwa ni njia Moja ya watoto hao kuendelea kutenda makosa Kila siku.

     "Sioni sababu ya watoto wanaotenda makosa kupewa msaada wa kisheria  kwani nao wanajielewa na wakisaidiwa  kisheria yaani watoto watakuwa wanajiamini Sana" Wamesema baadhi yao.

      Mtumwa Ameir Ali msaidizi wa sheria kutoka wilaya ya mjini amesema bado baadhi ya  wanajamii hawajaelewa kuhusu kutolewa Kwa msaada wa kisheria Kwa watoto wanaokinzana na sheria.

      Amesema ushawishi wao ni mkubwa Kwa kutafuta wakili wa usimamizi wa kesi za watoto pamoja na wao kumpa elimu na ushauri ili asirudie tena kosa Lile.

     Amefahamisha kuwa kumuacha mtoto aliekinzana na sheria ni kumkosesha haki zake za msingi ikiwemo kusoma pindi tu atakapokaa chuo Cha mafunzo Kwa Kukosa usaidizi wa kisheria.
    
     "Baadhi ya wajamii hawana uwelewa Kwa sababu wanaona yule mtoto ameshatenda Lile kosa kwanini sisi tunakaa tunamtetea lakini jamii hawajui kuwa Lile kosa linaweza kuwa lisiwe lake au amefanya kosa Kwa ule utoto tu." amesema.

     Bi mtumwa amesema ijapokuwa wao sheria inawabana kuingia mahakamani lakini hawawezi kumuacha mtoto aliekinzana na sheria hivyo wanaanza ngazi za awali ikiwemo polisi ili apate haki yake Kwa wepesi na haraka. 

    Jumla ya kesi 129 zimeripotiwa katika mahakama tofauti visiwani Zanzibar kuanzia January Hadi November 2023 zinazowahusu watoto waliokinzana na sheria ,  Kwa mujibu wa kitengo Cha TAKWIMU Dawati la Jinsia Makao Makuu ya polisi Zanzibar.

    Ambapo kesi 70 ni Kwa mkoa wa mjini magharib, 8 mkoa wa kusini unguja, 21 Kwa mkoa wa kaskazini unguja, 16 Kwa mkoa wa kusini Pemba na kesi 14 Kwa mkoa wa kaskazini Pemba.

   Akizungumza na mwandishi wa makala hii mratibu  wa Dawati la  jinsia makao makuu ya polis Zanzibar Sajent Rahma Ali Salum amesema watoto wanaokinzana na sheria wanawaangalia kama watoto wengine hasa katika kuwasaidia Kwa kuwapatia elimu ya kujitambua.

   Amesema  katika usaidizi wao wa kisheria Kwa watoto wa namna hii wanashirikiana na wasaidizi wa sheria, waratibu wa shehia pamoja na ustawi wa jamii  Kwa kusikiliza kesi zao Kwa  pamoja.

     Sagent Rahma amefahamisha kuwa  ni wajibu wa watoto wanaokinzana na sheria kupatiwa msaada kutokana na mazingira yanayojitokeza wakati wanapofanya makosa.

    "Tikifuatilia kesi zao nyingi ni ushawishi wa watoto wezao, wengine kuwa na njaa kutokana na Kukosa chakula nyumbani ilimradi makosa yao mengi ni ya ushawishitu" Amesema Sagent Rahma.

   Amesema Dawati la jinsia wanapopokea kesi za watoto waliotenda makosa wanawaita wazazi wao kuwafahamisha namna ya kukaa na mtoto wake kwani wazazi wengi huwachukia watoto wao kutokana na makosa yao.

   " Msaada wa kisheria Sana wanapewa na wasaidizi wa sheria wanakuwa pamoja na wazazi wao sisi tunawafahamisha namna Yale makosa yalivyo na mtoto akaenae vipi Kwa sababu wazazi wengine  wanakuwa wakali na kimchukia "Amesema.

       Amefahamisha kuwa katika kuwasaidia watoto wamekuwa wakipelekwa katika mahakama ya watoto ili wapate uhuru wa kujieleza mbele ya mahakama.

    Jumuiya ya wanasheria wanawake Zanzibar ZAFELA ni jumuiya isiyo ya kiserikali ambayo inatoa msaada wa kisheria Kwa wanawake na watoto imesema Kuanzia January Hadi November 2023 jumla ya kesi 11 za watoto wanaokinzana na sheria  zimefika ofisini kwao na wameanza  kuzishughulikia Kwa kuwapatia msaada wa kisheria na kesi 3 tayar zimeshapatiwa ufumbuzi Kwa kutozwa faini.

   Mwanaisha Mustapha ni mwanasheria kutoka jumuiya ya wanasheria wanawake Zanzibar ZAFELA amesema Kwa watoto wanaokinzana na sheria wamekuwa wakiwasimamia Kwa hali ya juu kwani wengi wao makosa yao ni ya kusingiziwa au ya kulipiziwa visasi Kwa baadhi ya wanajamii waliomzunguka.

    Amesema wao kama wanasheria wanasimama kwenye sheria ya mtoto inavyozungumza katika kumlinda kama mtoto mwengine mpaka pale mahakama itakapomtia hatiani Kwa kosa Lile.

    Amefahamisha kuwa hali ya Sasa asilimia kubwa watoto Kwa watoto wanafanyiana udhalilishaji jambo ambalo wanataasisi zinazotoa msaada wa kisheria wamekuwa macho ili  jamii ibaki kuwa salama.

   "Ni janga kubwa hali ya udhalilishaji na hali ya Sasa hivi iliokuwepo asilimia kubwa watoto Kwa watoto ndio wengi ambao wanafanya haya matukio Kwa iyo tukiwaangali kisheria wote ni watoto na wote wanataka kulindwa na sheria" Amesema mwanasheria.

    Shirika la msaada wa kisheria nà haki za binaadam  Zanzibar ZALHO kupitia wakili wake bi Jamila massoud  amesema jumla ya kesi 19 wanazishuhulikia katika shirika lao huku kesi 7 zikiwa zimeshafikishwa mahakamani Vuga zinazowahusu watoto wanaokinzana na sheria.

    Amesema  shirika limekuwa na utaratibu wa kuandaa mikutano na wanajamii ili kuzungumza nao na kuwafahamisha kwanini watoto waliokinzana na sheria wanatakiwa kupatiwa msaada wa kisheria.

   Amebainisha kuwa pale wanaposhughulikia kesi za watoto wanaokinzana na sheria wanashauri Sana kubadilishiwa makaazi pale anapokuwa tayar ameshakuwa mtoto mwema kwenye jamii ili asirudia tena makosa yale.

    "Tunawapa muelekeo au tunawapa utaalamu kwanini tunawasaidia hawa watoto Kwa sababu hawa ni Victim wa udhalilishaji ukiangalia mtoto anaekinzana na sheria utagundua kuwa nae kadhalilishwa Kwa namna Moja au nyengine" Amesema.

      Mohd Khamis Faki mkaazi wa kazole anaemlea mtoto wa dada yake  ajulikanae Kwa jina Khamis Mwadini Kheir mwenye umri wa  miaka 16 alishtumiwa Kwa kosa la kukashifu mtoto wa kike mwenye umri wa miaka 16 mnamo mwezi wa march 2023 huko maeneo ya Daraja bovu wilaya ya maghari A unguja.

     Katika shtaka Hilo lililopekea kufikishwa kituo Cha polisi Mwera na kesi kupelekwa mahakamani Vuga mjini unguja, ndugu Mohd Khamis amesema baada ya kufikishwa mahakamani shtaka la mjomba wake awali walishindwa Kwa Kukosa wakili kutokana na hali yao ya kimaisha.

      "Tulipandishwa mahakamani Vuga tulishindwa kupata wakili kutokana na hali zetu ndipo tukaunganishwa na Mtu kwenye hili shirika hili pale mikunguni linalosaidia watu wasio na uwezo na Kwa uwezo wa Mwnyezi Mungu Lile shirika lilitusaidia mpaka kesi ilipomalizika na alhamdullillah hatukutozwa  ushuru wowote ule" Ameongeza

      Amesema msaada walioupata kutoka shirika la ZALHO ni mkubwa kwani walishindwa na fedha za kuwapa wakili ili kuwasaidia kesi ya mjomba wake na Kwa Sasa mjomba wake huyo yupo huru na amejifunza kutokana na kosa Lile pamoja na kimkataza kufika katika mtaa aliopatia mtihani huo.

     "Kwa Sasa tumempiga Marufuku kufika mitaa ya Daraja bovu ambako ndipo alipo huyo binty kwenye hiyo nyumba aliofika mjomba wangu na Kwa Sasa hata hasogei kwani ulikuwa ni mtihani tu ule kwake" Amesema.

    Wizara ya Màendeleo ya jamií, jinsia wazee na watoto Zanzibar imesema hali ya upatikanaji huduma kisheria Kwa watoto ni ndogo na ndio maana wameona Kuna haja ya kutia mkono sheria iliopo Sasa ili kuboreshwa Kwa huduma.

   Mkuu wa Division ya hifadhi ya mtoto idara ya ustawi wa jamii na wazee ndugu sheikh Ali Sheikh amesema watoto wanaokizana na sheria sheria bado inamtanzama kama mtoto mbali ya kuwa wanatenda makosa lakini sheria inataka kuwalinda pia na kupewa haki zao.

   Amesema kama idara inatoa msaada wa kisheria Kwa kuwasimamia mahakamani hadi pale hukumu zinapotokea ambazo kikawaida ni kutozwa faini tu na sio kufungwa baadae idara inawapeleka vituo vya kurekebisha tabia kwenda kupata ujunzi na kujiweka sawa.

   "Tunamsaidia kama mtoto kama sheria inavyotaka atizamwe Kwa hiyo Kuna maafisa wetu mahakamani kuhakikisha juu ya kesi zao kama watenda makosa lakini mwisho wa siku Sheria inataka iwalinde" amesema.

    Kwa mujibu wa Wizara husika, taasisi za usaidizi wa sheria, waratibu na wadau mbali mbali mbali, suala la usaidizi wa sheria linahitaji kupewa kipaumbele Zaid huku wazazi nao wakitakiwa kusimamia msingi mzima wa malezi Kwa watoto wao ili kupatikana kizazi chenye maadili mazuri.

MWISHO..........0772694778





Tuesday, 17 October 2023

WADAU WA KUPINGA VITENDO VYA UDHALILISHAJI WAIJADILI SHERIA YA MTOTO NAMBARI 6 YA MWAKA 2011



Na Yassir Mkubwa EL BAHSAANY

Wadau wa kupinga Vitendo vya Ukatili na Udhalilishaji wa kijinsia wamesema Sheria ya Mtoto namba 6 ya mwaka 2011 ni vyema ikatambua mgawanyo  wa haki za watoto kwa kuzingatia umri ili kulinda maslahi na ustawi wa mtoto.

Wito huo umetolewa na na Hakimu dhamana Mkoa wa Kusini Unguja ndugu Khamis Rashid Khamis  Mara baada ya kikao  cha Mapitio cha  kujadili  sheria ya Mtoto na kutoa maoni kilichofanyika katika ukumbi wa kidongo chekundu Mental.

Amesema ni wakati sahihi  wa kueka sheria ambayo Itatoa muongozo wa kushughulikia watoto wenye umri wa chini ya miaka 14  na 16 na kuweka utaratibu wa kusikiliza kesi zao.





Hata hivyo amependekeza  suala la kueka sheria kwa skuli zinazolea watoto kuhakisha wanaimarisha mfumo wa kuieka saikolijia ya mtoto mhanga wa matukio mbali mbali nchini.

Mkurugenzi Idara ya Maendeleo ya Jamii,Jinsia Wazee  na Watoto ndugu Siti Abas Ali amesema umuhimu wa marekebisho ya Sheria ya  mtoto ni pamoja na maendeleo ya sayansi na teknolojia  ambayo kimsingi yameongeza haja ya kuimarisha baadhi ya vipengele vyake.

Aidha Mkurugenzi Siti amesisitiza suala la ushirikiano na wadau mbali mbali katika katika mapambano ya ukiukwaji wa haki za mtoto.

Amesema Wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto ipo tayari kushirikiana  na wadau hao  ili kufanikisha azma ya kuleta ustawi wa mtoto.

Baadhi ya wanasheria wamesema kikao hicho ni miongoni mwa sheria yoyote ni kutekeleza hivyo uwepo wa Ushirikishwaji wa wadau hao utasaidia kuleta ufanisi wa kiutekekelezaji wa sheria hiyo.

Wizara ya Maendeleo ya jamii jinsia Wazee na watoto inaendelea na ukusanyaji wa maoni ya sheria ya hiyo kwa lengo la kuipata sheria mpya na iweze kudumu kwa muda mrefu.

MWISHO